EDSON MWASABWITE: NI KWA NEEMA TU

Saturday, May 3, 2014

MWIMGBAJI GRACE CHRISTINA RWEGASHA (MCHUNGAJI MTARAJIWA) AMUA KUFUNGUKA NA KUELEZEA MAISHA YAKE NA HASA MAISHA YA WAIMBAJI NA WANANDOA YALIVYO KWA SASA


Kuna mambo mengi utaenda kujua kupitia mwimbaji huyu wa nyimbo za Injili Tanzania, Grace Rwegasha. Mwimbaji huyu haimbi peke yake bali anashirikiana na mdogo wake Joshua (Joshu).  Ngoja tusome haya mahojiano yaliyofanyika katika ofisi ya Rumafrica hapa Afrikasana Dar es Salaam Tanzania

Rumafrica: karibu sana katika ofisi zetu za Rumafrica, tunaomba ujitambulishe.

Grace Rwegasha: Nashukuru sana ndugu mtangazaji kwa kunikaribisha katika ofisi yako ili kuweza kujieleza, kwa jina naitwa GRACE RWEGASHA, katika huduma hii nimeimba na mdogo wangu anaitwa JOSHUA RWEGASHA ambaye sipo naye hapa yupo Mwanza anamalizia masomo yake ya University ST. AGAST.

Grace Christian Rwegasha

Rumafrica: Ni aina gani ya music mnapiga?
Grace Rwegasha: Sisi tunaimba nyimbo za Injili, mdogo wangu JOSHUA anakipaji cha uimbaji na anapenda kuimba kwa lugha ya kingereza. Toka akiwa mtoto alikuwa anapenda kuimba, anatunga nyimbo na baada ya kuwa mkubwa aliweza kuniambia dada twende tukarekodi, kwa hiyo ni huu mwezi wa nne ndio tumerekodi albamu yetu ya kwanza.

Rumafrica: Albamu yenu inaitwaje?


Bloga Rulea Sanga wa Rumafrica

Grace Rwegasha: Albamu yetu inaitwa MY SAVIOUR GOD
.
Rumafrica: ni lini ulianza hudua hii ya uimbaji wa nyimbo za Injili?

Grace Rwegasha: kwa kweli kuimba kupo kwenye damu yangu, wakati mwingi napenda kusifu na kuabudu, kwa hiyo kipaji cha kuimba ni kitu ambacho kilikuwa moyoni mwangu, lakini nilikuwa sijajipanga kwenda kujitokeza kwa watu kuimba, lakini mdogo wangu ndiye aliyenivuta akasema dada twende tukarekodi. Sijawahi kuimba kwenye kwaya yoyote lakini mimi mwenyewe tu nilikuwa napenda kuimba.

Rumafrica: Ni siku gani ambayo mliingia rasmi studio kwenda kurekodi?

Grace Rwegasha: Siku ambayo tuliingia studio rasmi kwenda kurekodi ilikuwa ni mwezi wa kwanza kwa huu 2014. Mdogo wangu JOSHUA alisema kwamba kuimba kumetawala sehemu kubwa ya maisha yake kwa sababu muda mwingi anautumia kwenye kutunga nyimbo, nyimbo zake zinafika zaidi ya elfu tano, kwa hiyon twende tukarekodi.

Rumafrica: kwa nini albamu yenu inaitwa MY SAVIOUR GOD?

Grace Rwegasha: Albamu yetu tulipenda kuiitwa MY SAVIOUR GOD kwa sababu pia kuna wimbo unaitwa My Seviour God, nakumbuka siku ya huo wimbo Joshua aliamka alfajiri sana akaniambia Grace mimi nimepata wimbo, mimi nilijua kwamba wimbo huo ameshushiwa kutoka juu mbinguni kwa hiyo wimbo huo tukaupa jina la MY SAVIOUR GOD, Mungu anakwenda kutuinua kupitia wimbo huu.

Rumafrica: Albamu yenu inanyimbo ngapi?

Grace Rwegasha: Albamu yetu kwa sasa ina nyimbo 12, tuliamua tufanye nyimbo 12 kwa sababu tulipofikia kutaka kutoa Albamu watu walituambia kwamba nyimbo zetu hazitanunuliwa kwa sababu watu wengi huwa hawapendi nyimbo za kingereza. Lakini sisi tukasema sasa tufanyeje kwa sababu Mungu anatushushia nyimbo za kingereza, tukaona kwamba tukiziacha itakuwa ni kama mtu umewasha taa alafu ukaiweka chini ya uvungu wa kitanda. Ndipo tulienda studio kurekodi lakini tukaamua tuchanganye kwa hiyo tumefanya 9 kiswahili na 6 kingereza.

Rumafrica:
Tungependa kujua majina ya nyimbo zilizopo katika Albamu yenu?

Grace Rwegasha: Nyimbo zilizopo kwenye albamu yetu majina yake ni MTENDA MIUJIZA, GEUKA, YUHAI, MJI WA MUANGAZA. Na za kingereza kuna MY SAVIOUR GOD, ALL MY HAND, PARADISE.

Rumafrica: ni nyimbo gani unaipenda sana katika albamu yenu?

Grace Rwegasha:
Wimbo ambao ninaupenda sana ni MY SAVIOUR GOD, ni wimbo ambao unanigusa sana katika moyo wangu, pia ninaupenda wimbo wa TENDA MIUJIZA, kwa kweli Bwana anatenda miujiza mpana nimefikia kuimba hiyo ni miujiza.

Rumafrica:
Style gani ya uimbaji mnatumia?

Grace Rwegasha: style zetu tumechanganya, nyimbo nyingine tunaweza tukacheza Quito, nyingine tunaweza tukacheza Charanga, kwa hiyo tumechanganya changanya hatujacheza katika style moja. Kwa kweli tumependa kufanya hivyo kwa sababu ili tuweze kufafuraisha watu zaidi, kwa mfano utakuta kuna yimbo ya harusi, nyimbo ya kuabudu.

Rumafrica:
Tungependa kusikia akapela ya wimbo mmoja.

Grace Rwegasha: Naomba niimbe wimbo wa MTENDA MIUJIZA:…… Yupo mtenda miuujizaa, yupoo yupoo, yupo na atakuwepo, yupooo yupooo, Yesu wa kabila la Yudaaa, mwana wa Mungu aliye haii, Yesu wa kabila ya Yuda mwana wa Mungu aliye haiii.

Rumafrica:
ni studio gani mmerekodi nyimbo zenu?

Grace Rwegasha: Nyimbo zetu tumerekodia kwa produce anaitwa RICK, kwa kweli huyu produce amekuwa mtu mzuri sana kwangu, alitupokea vizuri tulikuwa tunakatishwa sana tamaa kwamba nyimbo za kingereza hazitanunuliwa lakini produce Rick akasema hapana Watanzania wanapenda sana nyimbo za kingereza na nyimbo zenu ni nzuri mtafika nazo mbali. Na pia alitushauri tutunge na nyimbo za Kiswahili japokuwa zilikuwa chini ya kiwango, basi tuliweza kutunga mpaka zikafikia nyimbo 9.

Rumafrica:
Watu wanasema nyimbo za kingereza hazina upako kwa Watanzania, unasemaje?

Grace Rwegasha:
mimi ninaujasiri mkubwa sana kwamba Watanzania wanapenda nyimbo za kingereza, labda sisi Watanzania hatujafikia kiwango cha kuweza kutunga nyimbo za kingereza tunajaribu jaribu, lakini kwa mtazamo wangu Watanzania wanapenda nyimbo za kingereza.

Rumafrica:
Changamoto gani mnazipata katika huduma yenu ya uimbaji?

Grace Rwegasha: Changamoto tunazozipata ni nyingi hasa kwa marafiki ambao nilikuwa nao kabla sijaenda studio, ukiwaomba ushauri wanakwambia wewe sauti yako sio nzuri usiende, wengine wananiambia wewe nenda katafute shamba ulime, wengine wananiambia nenda kafuge kuku kwani hautaweza kuimba. kwa hiyo ukisikiliza watu unaweza usifikie lile lengo ambalo Mungu anataka ulifanye, kwa hiyo hizo ndo changamoto na kama nilivyotangulia mwanzo kusema walikuwa wanatukatisha tamaa kuimba nyimbo za kingereza, nilichojifunza ni kwamba sikiliza Roho wa Mungu anakwabia fanya nini. Pia kuna studio moja ambayo tulienda, kwa kweli produce alitutesa sana, tulimpatia fedha tukarekodi nyimbo, lakini fedha nyimbo mpaka leo hatujaviona, na dhani ni miaka 2 sasa imepita, lakini sisi tumemsamehe ila tu hizo nyimbo zetu asije akazitoa popote. Kwa hiyo ni changamoto mbaya sana ambayo tuliipitia kabla hatujakutana na huyu Produce Rick.
Rumafrica: Je mlichukuwa hatua yoyote kwa huyu aliyewatapeli fedha zenu za studio?
Grace Rwegasha: kwa kweli tuliwaza sana kuhusu hilo, lakini tukaona kwamba kwa sababu sisi tulitaka kumtumikia Mungu, na hichi kitu ni cha kumtumikia Mungu, huwenda sio yeye aliamua kufanya hivyo bali ni shetani, kwa hivyo sisi tukiamua kumchukulia hatua tutakuwa tukipigana na mtu badala ya kupigana na shetani, na ili tuweze kumshinda shetani tuliamua kumsamehe.

Rumafrica:
Jamii imefaidika nini na huduma yenu?

Grace Rwegasha:
Huduma yetu ndo tumeanza, tunaimani Mungu atatubariki na ipo siku atatupa kitu mkononi cha kuweza kuisaidia jamii, kwa sasa tumetoa nyimbo ili watu wapokee kwaajili ya Roho zao.

Rumafrica: Kwa nini waimbaji wanatanguliza pesa na huduma baadaye?

Grace Rwegasha:
ni kweli, ila kwa sasa hivi inabidi waimbaji tubadilike kwa sababu tumejiachia sana, tumesahau kuwa sisi ni watumishi wa Mungu tumeenda kibiashara zaidi. Kwa mfano biblia inasema mmepata bure toweni bure, ndio najua mwimbaji anategemea pale ndio atakula na kufanya mambo yake mengine lakini Bwana Yesu anasema tumtegemee yeye kwa kila jambo na yeye atafanya. Kwa hiyo inabidi mtu anapoitwa asiweke kiwango cha fedha ndio akatoe huduma, kama tumeamua kumtumikia Mungu basi tumtumikie Mungu kweli nayeye atatubariki.

Rumafrica: Unasemaje juu ya hawa wanaotegemea uimbaji?

Grace Rwegasha: Mimi ninafikiri hilo kwa sababu na Wachungaji nao wanajua ni watoto wadogo ambao Bwana anawainua na wanategemea hivyo watawapa zawadi. Lakini mimi kitu ambacho naweza kupinga ni pale ambapo mchungaji amekuita uende kuimba akakwambia nitakupa kiasi kadha cha fedha mwambie mchungaji asante mimi nakuja, lakini kitendo cha kukataa na kusema hapana bila kufikisha milioni 5 mimi siji, kwa kweli hapo tunakuwa tunamkosea Mungu.

Rumafrica: Kwa nini ndoa za waimbaji hazidumu?

Grace Rwegasha: Kwa kweli hilo swali ni gumu sana kulijibu, ila ngoja niseme mimi kwa mtazamo wangu, mtu yeyote Yule ambaye ni mtumishi shetani utafuta njia nyingi sana za kuweza kumwangusha, shetani akikukosa kwenye pombe lazima atatafuta pale ambao mpo waili kwenye ndoa, au kwenye udhaifu ni wapi, kwa hiyo shetani utafuta mbinu na kila namna ili tu avuruge. Kwa mfano labda mama umeachwa nyumbani badala ya kuamini kwamba baba ameenda kuhubiri, au mume wangu ni mwimbaji na ameenda kuimba kweli wewe unaanza kuwaza tofauti kwa sababu pia shetani uingia kwa njia ya mawazo, kwa hiyo unavyowaza vile na shetani naye hupata nafasi ya kuweza kuvuruga ndoa yako. Kwa hiyo inabidi pia tuwe waombaji ili tuweze kumshinda shetani.

Rumafrica: Ni kwa nini mchungaji anatenda maovu mitaani lakini bado anakuwa na upako wa miujiza madhabahuni?

Grace Rwegasha: Mimi ninachopenda kusema ni kwamba jina Yesu lenyewe linajitegemea, ila Mungu wetu ni Mungu mwenye huruma na rehema nyingi, kwa hiyo ukimuona mchungaji ameenda katika njia ambazo sizo ujue bado yupo katika mkono wa Mungu wenye rehema. Kwa sababu Mungu hapendi mtu Yule apotee aende jehanamu
.
Rumafrica: Unasemaje juu ya watumishi wanaokamatwa na maovu na baada ya kukamatwa wanakimbilia nchi nyingine na kuanzisha huduma huko?

Grace Rwegasha: Mimi ninachopenda kusema ni kwamba hautakiwi kukimbia, bali unapaswa kutubu mbele za Mungu wako na mbele za watu, na uwe umedhamiria kuomba toba ya kweli maana Mungu anaangalia ndani ya moyo. Unaweza ukasema mbele za watu mnisamehe kumbe wewe hujafanya toba ya kweli na Mungu wako, kwa hiyo ukifanya toba ya kweli na Mungu atauondoa ule uovu, kwa hiyo utakuja kushangaa kwamba watu hawata libeba lile jambo kwa huzito kama ambavyo ungefikiria kukimbia. Lakini endapo utakimbia huko unapoenda nako Mungu anakuangalia unafanya sawa au sio sawa, na mpaka ufika hiyo nchi nyingine ni jambo la kumshukuru Mungu kwa sababu ungeweza ukafia njiani, kwa hiyo kuna haja ya kutubu na kumrudia Mungu.

Rumafrica: Unasemaje juu ya watu wanaotangatanga mara wamwimbie Mungu na mara waimbe nyimbo za kidunia na sio za Mungu?

Grace Rwegasha: Ukisoma katika kitabu cha Waebrania 10:26…, Biblia inasema: Maana kama tukifanya dhambi kusudi baada ya kupokea ujuzi wa ile kweli, haibaki tena dhabibu kwaajili ya dhambi, bali kuna kuitazamia hukumu yenye kutisha, na ukali wa moto ulioyatayari kuwala wao wapingao, mtu aliyeidharau sheria ya Musa, hufa pasipo huruma kwa neno la mashahidi wawili au watatu … Napenda kuwaonya kwa Roho mtakatifu wale ambao wanapenda kufanya hivyo waache, wamtumikie Mungu katika Roho na kweli, maana hapa duniani sio petu, utajiri tunaoutafuta hautatufikisha popote, hata ukijenga majumba utayaacha, tengeneza kwanza kwaajili ya ufalme wa Mungu. Kwa kweli mimi ninafuraha sana kwa wale wanaotoka katika nyimbo za kidunia na kumuimbia Mungu, kwa sababu Yesu mwenyewe anasema mimi ndiye njia ya kweli na uzima, mtu aji kwa baba isipokua kwa mimi yaani Yesu Kristo. Na yeye Yesu ndiye mlango kwa hiyo sisi kama waimbaji wa nyimbo za Injili tunamwimbia Kristo na ili watu wengine waje katika huu mlango.

Rumafrica: Asante sana kwa kuwa na wewe na karibu sana katika office zetu za Rumafrica, na Mungu akubariki sana katika karama yako ya uimbaji, na naimani Mungu atakuinua sana utatoka hapo na utakuwa muhubiri.

Grace Rwegasha: Halleluya, namuomba Mungu anipe hiyo nafasi.

UNAWEZA KUWASILINA NAYE KWA SIMU +255 788 443 346

No comments:

Post a Comment